BUNGE LA MTAA
Ni blog inayohusu masuala muhimu kwa maendeleo ya Taifa Letu ya kisiasa na kijamii, karibu tujadiIlane.
Wednesday, 2 March 2016
SHETTA AFUNGUKA KUHUSU GARI LAKE, NA KITENDO CHA KUIGIZWA AKISHIKWA MAKALIO
Baada ya msanii Nay wa Mitego kuachia wimbo wake wa shika Adabu Yako yamesemwa mengi katika mtandao ya kijamii, kutokana na msanii huyo kutumia kipaji chake kuwachana mastaa mbalimbali hapa Bongo akiwemo Shilole, Snura, Wema Sepetu, Ray, Niva, Shetta na wengine wengi.
Wednesday, 27 May 2015
MTOTO WA BABA WA TAIFA AONESHA NIA YAKE YA KUGOMBEA URAIS
Kupitia urasa wake wa Facebook Charles Makongoro Nyerere ambaye ni mtoto wa hayati baba wa taifa Mwalimu JK Nyerere
ameandika ujumbe mfupi ulioambatana na taarifa kwa vyombo vya habari kuhusu nia yake ya kutaka kugombea urais kupitia tiketi ya chama cha mapinduzi CCM
Ndugu zangu watanzania, taifa letu lipo kwenye mchakato wa uchaguzi, mchakato huu ni msingi mkubwa wa maamzi kwa ajili ya maendeleo ya taifa letu. Tunaamua hatma ya taifa letu kwa miaka mitano ijayo. Ni kwa sababu hii mimi Charles Makongoro Julius Nyerere nawakaribisha rasmi kijijini kwetu Mwitongo Butiama, Mara.tarehe 1/6/2015 kuwaelezeni nia yangu ya kuomba ridhaa ya wanaccm nafasi ya kupeperusha bendera ya ccm kuliongoza taifa hili kwa nafasi ya urais.
ameandika ujumbe mfupi ulioambatana na taarifa kwa vyombo vya habari kuhusu nia yake ya kutaka kugombea urais kupitia tiketi ya chama cha mapinduzi CCM
Ndugu zangu watanzania, taifa letu lipo kwenye mchakato wa uchaguzi, mchakato huu ni msingi mkubwa wa maamzi kwa ajili ya maendeleo ya taifa letu. Tunaamua hatma ya taifa letu kwa miaka mitano ijayo. Ni kwa sababu hii mimi Charles Makongoro Julius Nyerere nawakaribisha rasmi kijijini kwetu Mwitongo Butiama, Mara.tarehe 1/6/2015 kuwaelezeni nia yangu ya kuomba ridhaa ya wanaccm nafasi ya kupeperusha bendera ya ccm kuliongoza taifa hili kwa nafasi ya urais.
Monday, 3 November 2014
MAKONDA: MSINIGOMBANISHE NA WARIOBA
![]() |
MH. PAUL MAKONDA |
Aliyekuwa mjumbe wa bunge maalum la katiba Mh.Paul
Makonda,amekanusha vikali
kuhusika na vurugu zilizotokea jana katika mdahalo ulioandaliwa
na Taasisi ya Nyerere Foundation, ambapo msemaji mkuu alikuwa jaji Joseph Warioba.
Makonda amesema hafahamu chanzo cha vurugu hizo na
hawajui watu walioanzisha vurugu hizo ila amewafananisha na wahuni wasioitakia
mema amani ya nchi
Makonda ameongeza kuwa amefedheheshwa na kitendo
cha kupigwa muandishi wa habari wa BBC Anord Kayanda ambaye alijeruhiwa
kichwani na mlemavu wa macho Amoni Mpanju.
Vilevile amelaani kitendo cha baadhi ya watu
kumgombanisha na Jaji Warioba na amesisitiza kuwa hana ugomvi na jaji huyo.
![]() |
MH.Jaji Warioba akiokolewa na aliyekuwa mjumbe wa bunge maalum la katiba Paul Makonda(aliyemshika kiunoni) |
Makonda ameendelea kusema kuwa ana mahusiano mazuri na jaji Warioba na
amewasiliana nae kumpa pole kwa kilichotokea na hakupigwa wala kujeruhiwa, na
amehoji kuwa inawezekana vipi kumpiga mtu siku moja kabla na mkaendelea kuwasiliana nae vizuri.
Friday, 19 September 2014
JUKWAA LA WAHARIRI:JESHI LIFUMULIWE.
Absolum Kibanda |
Ameyasema hayo kufuatiwa kupigwa kwa waandishi wa habari walipokuwa wakikusanya taarifa kuhusiana na kukamatwa na kuhojiwa kwa Mwenyekiti wa chama cha Demokrasia na Maendeleo ndugu Freeman Mbowe makao makuu ya jeshi la polisi jijini Dar es Salaam
![]() |
Askari wakimzonga mwandishi wa Habari |
Kibanda amelaani vikali kitendo hicho na kuwataka jeshi la polisi lijue umuhimu wa vyombo vya habari kwa jamii,
Pia ameongeza kuwa licha ya kulaani hawataishia hapo wataenda mbele zaidi ili kufanikisha wajibu na taaluma ya uandishi wa habari inaheshimiwa,
Pia watamuandikia barua mkuu wa jeshi la polisi Ernest Mangu juu ya kilichotokea na kusikiliza nini kitatokea,
Vilevile amezitaka taasisi nyingine ikiwemo ya haki za binadamu kulaani na kuwachukulia hatua walioonekana dhahiri wa wakifanya vitendo hivyo.
Thursday, 17 July 2014

Uhalifu huo unadaiwa kutekelezwa wiki mbili zilizopita.
Mtoto huyo alibakwa na mlinzi pamoja na mwalimu, lakini kwa sababu ya kuwepo walinzi wengi katika shule hiyo, polisi bado wanachukua muda kuchunguza mlinzi aliyehusika.
Polisi wanasema kuwa mtoto huyo alibakwa tarehe mbili Julai , lakini wazazi wake waligundua hilo siku chache zilizopita baada ya mtoto huyo kulalamika kuumwa na tumbo na kupelekwa hospitalini.
Wakati huo mamia ya wazazi wameandamana nje ya shule wakivunja milango na kupiga mayowe kulaani tukio hilo.
Wednesday, 16 April 2014
MAALIM SEIF ATOA KAULI 7 DHIDI YA MUUNGANO.
2.‘Ukitaka upate maenedeleo, yatambue mafanikio yako lakini
pia usisahau matatizo yako, ni ni moja.. kufanya vizuri, Sidhani katika
Tanzania kama kuna watu hawataki muungano, na kama wapo ni wachache, muungano
uendelee ndio la msingi’
3. ‘Sio dhambi watu kuwa na fikra tofauti, sio dhambi hata
kidogo kwa sababu hatuwezi wote kuwa na fikra aina moja, Wanaotaka serikali
moja wasibezwe, mbili wasibezwe, wanaotaka tatu na serikali ya mkataba
wasikilizwe pia’
4. ‘Wako wanaoamini kwamba matatizo ya muungano yako kwenye
muundo, tuwasikilize wana hoja gani, Mwaka 1963 Malaysia na Tanganyika
maendeleo ya sehemu zote hizi yalikua sawa, mwaka 2014 tujiulize, changamoto
kwetu ni vipi tutakua na muungano utakaokua ni chachu ya maendeleo ya haraka,
mambo ya 74 ni tofauti na 2014′
5. ‘Tuwe makini sana, sote ni wa nchi moja, tujiepushe na
kikundi chochote kuona wao wana haki zaidi, Watanzania wote sawa, wajumbe wa
bunge maalum waangalie maslahi ya nchi, muungano huu ni wa nchi 2 zilizokua dola
huru na kuungana kwa hiari
6. ‘Tupate katiba ambayo itaondoa migogoro, kero iwe ni
historia… hili swala lisiwepo tena, tusiende kwenye maamuzi ya harahaharaka
tukasema serikali mbili au tatu bila kuangalia athari zake, katiba ya Znz
inasema ni miongoni mwa nchi mbili za muungano, ya Muungano inasema Tz ni nchi
moja, huo ni mgogoro’
7. ‘Nadhani Warioba walivyopendekezwa waliona hisia za Znz
zilivyo, tunataka katiba itakayotambua usawa wa nchi mbili, hakuwezi kuwa na
katiba ambayo itamridhisha kila mtu lakini angalau wengi wao waridhike’.
Subscribe to:
Posts (Atom)