Absolum Kibanda |
Ameyasema hayo kufuatiwa kupigwa kwa waandishi wa habari walipokuwa wakikusanya taarifa kuhusiana na kukamatwa na kuhojiwa kwa Mwenyekiti wa chama cha Demokrasia na Maendeleo ndugu Freeman Mbowe makao makuu ya jeshi la polisi jijini Dar es Salaam
![]() |
Askari wakimzonga mwandishi wa Habari |
Kibanda amelaani vikali kitendo hicho na kuwataka jeshi la polisi lijue umuhimu wa vyombo vya habari kwa jamii,
Pia ameongeza kuwa licha ya kulaani hawataishia hapo wataenda mbele zaidi ili kufanikisha wajibu na taaluma ya uandishi wa habari inaheshimiwa,
Pia watamuandikia barua mkuu wa jeshi la polisi Ernest Mangu juu ya kilichotokea na kusikiliza nini kitatokea,
Vilevile amezitaka taasisi nyingine ikiwemo ya haki za binadamu kulaani na kuwachukulia hatua walioonekana dhahiri wa wakifanya vitendo hivyo.
No comments:
Post a Comment