Kupitia urasa wake wa Facebook Charles Makongoro Nyerere ambaye ni mtoto wa hayati baba wa taifa Mwalimu JK Nyerere
ameandika ujumbe mfupi ulioambatana na taarifa kwa vyombo vya habari kuhusu nia yake ya kutaka kugombea urais kupitia tiketi ya chama cha mapinduzi CCM
Ndugu zangu watanzania, taifa letu lipo kwenye mchakato wa uchaguzi, mchakato huu ni msingi mkubwa wa maamzi kwa ajili ya maendeleo ya taifa letu. Tunaamua hatma ya taifa letu kwa miaka mitano ijayo. Ni kwa sababu hii mimi Charles Makongoro Julius Nyerere nawakaribisha rasmi kijijini kwetu Mwitongo Butiama, Mara.tarehe 1/6/2015 kuwaelezeni nia yangu ya kuomba ridhaa ya wanaccm nafasi ya kupeperusha bendera ya ccm kuliongoza taifa hili kwa nafasi ya urais.


No comments:
Post a Comment