![]() |
MH. PAUL MAKONDA |
Aliyekuwa mjumbe wa bunge maalum la katiba Mh.Paul
Makonda,amekanusha vikali
kuhusika na vurugu zilizotokea jana katika mdahalo ulioandaliwa
na Taasisi ya Nyerere Foundation, ambapo msemaji mkuu alikuwa jaji Joseph Warioba.
Makonda amesema hafahamu chanzo cha vurugu hizo na
hawajui watu walioanzisha vurugu hizo ila amewafananisha na wahuni wasioitakia
mema amani ya nchi
Makonda ameongeza kuwa amefedheheshwa na kitendo
cha kupigwa muandishi wa habari wa BBC Anord Kayanda ambaye alijeruhiwa
kichwani na mlemavu wa macho Amoni Mpanju.
Vilevile amelaani kitendo cha baadhi ya watu
kumgombanisha na Jaji Warioba na amesisitiza kuwa hana ugomvi na jaji huyo.
![]() |
MH.Jaji Warioba akiokolewa na aliyekuwa mjumbe wa bunge maalum la katiba Paul Makonda(aliyemshika kiunoni) |
Makonda ameendelea kusema kuwa ana mahusiano mazuri na jaji Warioba na
amewasiliana nae kumpa pole kwa kilichotokea na hakupigwa wala kujeruhiwa, na
amehoji kuwa inawezekana vipi kumpiga mtu siku moja kabla na mkaendelea kuwasiliana nae vizuri.
Iko vizur kaka
ReplyDeleteamani ni muhimu muacheni Warioba afanye yake
ReplyDelete