Monday, 14 April 2014

BILAL, MAGUFULI, KOVA WANUSURIKA KIFO.

Taarifa za ajali hiyo zikiambatana na picha kadhaa za helikopta hiyo ya Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ), zilianza kusambaa kwenye mitandao ya kijamii na baadaye kuthibitishwa na Mkuu wa Majeshi (CDF), Jenerali Davis Mwamunyange.

Mwamunyange afafanua
Akizungumza na mwandishi wetu, Jenerali Mwamunyange alisema ajali hiyo ilihusisha helikopta ya JWTZ yenye muundo wa Agusta Bell (AB 412) iliyotengenezwa Italia.
Alisema helikopta hiyo ilipangwa kuwazungusha viongozi hao katika maeneo yaliyoathiriwa na mvua zinazoendelea kunyesha jijini Dar es Salaam na kusababisha maafa.
Jenerali Mwamunyange ambaye pia jana alitembelea baadhi ya maeneo yaliyokumbwa na mafuriko kuona kama kuna msaada wa haraka wa kijeshi unaohitajika, alisema helikopta hiyo, ilipata ajali punde tu baada ya kuruka na kugonga ukuta.
“Ni kweli kwamba helikopta iliyopata ajali inamilikiwa na JWTZ…Hiyo ni ajali kama ajali nyingine yoyote. Imekuwa ni bahati mbaya wakati inaanza kuruka ikagonga ukuta wa jengo na kushuka chini….Mpaka sasa hatujajua sababu ya ajali hiyo,” alisema.
Aliahidi kwamba uchunguzi yakinifu kuhusu chanzo cha ajali hiyo utafanyika kwa kuhusisha wataalamu. Alisema helikopta hiyo ilikuwa ni miongoni mwa usafiri wa kutegemewa jeshini na ilifanyiwa majaribio Jumamosi na jana asubuhi na haikuonyesha tatizo lolote na kwamba imekuwa ikifanya kazi kwa muda mrefu bila matatizo yoyote.
“Nilikuwa wa kwanza kuruka wakati waokoaji wakiendelea kuokoa wengine waliokuwa ndani,’’ alisema Kova na kuongeza: “Tunawashukuru sana wale waliokuwapo nje ya helikopta hiyo kwani walisaidia tukashuka salama na kuendelea na majukumu yetu ya Taifa kama kawaida.’

No comments:

Post a Comment