Taarifa za ajali hiyo zikiambatana na picha kadhaa
za helikopta hiyo ya Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ),
zilianza kusambaa kwenye mitandao ya kijamii na baadaye kuthibitishwa na
Mkuu wa Majeshi (CDF), Jenerali Davis Mwamunyange.
Mwamunyange afafanua
Alisema helikopta hiyo ilipangwa kuwazungusha
viongozi hao katika maeneo yaliyoathiriwa na mvua zinazoendelea kunyesha
jijini Dar es Salaam na kusababisha maafa.
Jenerali Mwamunyange ambaye pia jana alitembelea
baadhi ya maeneo yaliyokumbwa na mafuriko kuona kama kuna msaada wa
haraka wa kijeshi unaohitajika, alisema helikopta hiyo, ilipata ajali
punde tu baada ya kuruka na kugonga ukuta.
“Ni kweli kwamba helikopta iliyopata ajali
inamilikiwa na JWTZ…Hiyo ni ajali kama ajali nyingine yoyote. Imekuwa ni
bahati mbaya wakati inaanza kuruka ikagonga ukuta wa jengo na kushuka
chini….Mpaka sasa hatujajua sababu ya ajali hiyo,” alisema.
Aliahidi kwamba uchunguzi yakinifu kuhusu chanzo
cha ajali hiyo utafanyika kwa kuhusisha wataalamu. Alisema helikopta
hiyo ilikuwa ni miongoni mwa usafiri wa kutegemewa jeshini na ilifanyiwa
majaribio Jumamosi na jana asubuhi na haikuonyesha tatizo lolote na
kwamba imekuwa ikifanya kazi kwa muda mrefu bila matatizo yoyote.
“Nilikuwa wa kwanza kuruka wakati waokoaji
wakiendelea kuokoa wengine waliokuwa ndani,’’ alisema Kova na kuongeza:
“Tunawashukuru sana wale waliokuwapo nje ya helikopta hiyo kwani
walisaidia tukashuka salama na kuendelea na majukumu yetu ya Taifa kama
kawaida.’
No comments:
Post a Comment