
Takwimu hizo zilitolewa wilayani Chalinze na Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), Jaji Mstaafu Damian Lubuva, katika mkutano wa maandalizi ya uchaguzi huo uliohudhuriwa na vyama mbalimbali vya siasa.
Alisema tofauti ya idadi ya wapiga kura waliopo katika daftari la kudumu la wapiga kura kwa mwaka 2010 na daftari lililohakikiwa mwaka huu ni watu 80.
Alisema daftari la kudumu la wapiga kura kwa Jimbo la Chalinze lilikuwa na wapiga kura 92,859 kwa uchaguzi mkuu wa mwaka 2010.
Jaji Lubuva alisema wapiga kura waliokuwa wanaonekana katika daftari zaidi ya mara moja majina yao yameondolewa na wapiga kura walioandikishwa na wana kadi ya mpiga kura lakini hawaonekani katika daftari wameingizwa.
“Sababu zilizochangia wapiga kura kujitokeza mara nyingi ni wapiga kura kujiandikisha zaidi ya mara moja au wapiga kura kubadili taarifa zao wakati wa zoezi la uboreshaji wa daftari,” alisema.
Mkurugenzi wa Uchaguzi, Julius Mallaba, alisema siku ya uchaguzi ni marufuku kwa mgombea, chama cha siasa au wakala kufanya kampeni na kusema kwa mujibu wa sheria mwisho wa kufanya kampeni ni siku moja kabla ya siku ya uchaguzi yaani Aprili 5, mwaka huu.
No comments:
Post a Comment